Powered by Blogger.

Wikipedia

Search results

Translate

You are here: Home / HATIMAYE LOIS VAN GAAL KAWA COACH MAN UNITED

HATIMAYE LOIS VAN GAAL KAWA COACH MAN UNITED

| No comment

20140519-205528-75328737.jpg

 Hatimaye Louis van Gaal ameteuliwa na kuthibitishwa kuwa kocha mpya wa Manchester United.
Van Gaal (62) ambaye ni Kocha wa Timu ya Taifa ya Uholanzi amesaini mkataba wa miaka mitatu na Ryan Giggs atakuwa msaidizi wake, akihitimisha kipindi chake cha soka ya kulipwa.
Van Gaal anachukua nafasi iliyoachwa na David Moyes aliyefukuzwa kazi baada ya miezi 10 kutokana na kushindwa kuvaa viatu vya David Moyes.
Mdachi huyu amepata kutwaa ubingwa alipowafundisha Ajax wa Uholanzi, Barcelona wa Hispania, Bayern Munich wa Ujerumani na AZ Alkmaar wa nchini mwake.

Anatarajiwa kuingia Old Trafford baada ya kumaliza mkataba wake kwenye Kombe la Dunia ambako atawaongoza Uholanzi, akiwamo mshambuliaji wa Man U, Robin van Persie.
Amejigamba kwamba amepata kusimamia mechi Old Trafford na anajua palivyo kwa hiyo hana wasiwasi atakapoanza kazi hapo na kwamba anawasoma vyema washabiki wa klabu hiyo aliyosema ni kubwa zaidi duniani.
Amesema kwamba ilikuwa ndoto yake siku zote kufanya kazi na moja ya klabu za Ligi Kuu ya England na ana uhakika kwa ushirikiano na wenzake wataweka historia mpya.
Naibu Mwenyekiti wa Man United, Ed Woodward amesema kwamba baada ya zahama ya Moyes, anaamini kuwa amemteua mtu sahihi kwa kazi hiyo kwa sababu historia yake inaonesha mafanikio makubwa.